Breaking News
recent

RAMMY KUIGIZA NA AKI NA UKWA.

 Msanii wa Filamu za Bongo Rammy Galis, ameweka wazi kisa cha Filamu anayokwenda kushiriki nchini Nigeria Mwisho wa mwaka huu na Wachekeshaji wakongwe Aki na Ukwa.

Akizungumza Rammy alisema kuwa,  ataigiza kama Shemeji wa Wachekeshaji hao wawili ambaye hana Mkwanja na amesafiri mpaka Nigeria kwenda 'Kumchuna' Dada yao.

"Story iko hivi Aki na Ukwa ni mashemeji zangu lakini sina kitu Ila Nina mapenzi ya kweli, sasa nimesafiri mpaka Nigeria kwenda kumfata Dada yao na nimefikia nyumbani kwao, kwa hiyo Aki na Ukwa wananifanyia vita ili nirudi Tanzania kwa kuwa sina kitu, wanamtafutia Dada yao Wanaume wenye pesa"

" Ila kikwazo ni Mimi kwa kuwa Dada yao ananipenda sana, kwa hiyo wananifanyia visa vingi Mara maneno Mara nafungiwa nje Dada yao akienda kazini yaani ni Taflani Mtindo mmoja" alisema Rammy Galis.


Katika hatua nyingine Staa huyo wa Filamu ya Chausiku, amedai Japokua anafahamu wapo baadhi ya wasanii ambao hawaonyeshi kufurahishwa harakati hizi lakini itabidi tu wakubali, Rammy ndio anaweza kuwa ngazi ya kwanza  katika kuipeperusha bendera taifa letu katika tasnia ya filamu.

Na Brighiter  Masaki.

No comments:

Powered by Blogger.