Breaking News
recent

MR UNIVERSE MATUKIO ATANGAZA FURSA KWA VIJANA

MR Universe Tanzania mwaka 2002,Matukio Chuma,amewataka vijana  wa Kitanzania kutumia fursa  mbalimbali  zinazojitokeza ndani na  nje ya  nchi kuliko kulalamika kuwa hakuna fursa.

Akizungumza na waandishi,,katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere uliopo jijini Dar es salaam,
baada ya kuwasili  akitokea Marekani ambako ndiko anapofanyia  shughuli zake za uandishi wa  vitabu na  mashairi, ujasiriamali uhamasishaji, Chuma alisema kuwa sasa ni wakati wa vijana wa Kitanzania kuthubutu  na  kutumia  fursa mbalimbali ambazo zimekuwa zikitangazwa duniani.

“Nawashukuru watu wote waliojiokeza na  kwamoyo wa upendo walionionyesha, baadhi ya marafiki zangu kwa kuja kunipokea, ushauli na kilio change ni kwa vijana wenzangu wa Kitanzania ni kuthubutu na  kutumia fursa  mbali mbali  ambazo zimekuwa zikitangazwa duniani kama ambavyo mimi nilithubutu na ninazidi kuendelea kuthubutu ndio siri kubwa ya mafanikio yangu”alisema Chuma

Aidha Chuma aliongeza kwa kusema kuwa yeye  yupo eyali kwa kijana yeyote wa kitanzania ambaye ataitaji  msaada wa kupata Fursa yupo ayari kumsaidai bega kwa bega katika kufanikisha ndoto zao.

Na Brighiter Masaki


No comments:

Powered by Blogger.