Breaking News
recent

BEN POL ATAJA SIFA ZA MWANAMKE ANAEMUITAJI.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya  nchini Ben Pol amesema kitu pekee anachokiangalia kwa mwanamke ambaye ataweza kumpenda  na kuwa naye na mahusiano ya kimapenzi ni lazima awe anajiamini pindi wakiwa wanaongea au hata wakiwa wanachati.


Ben Pol amefunguka hayo baada ya kupita siku chache, aliyekuwa anadaiwa kutoka naye kimapenzi ambaye ni msanii wa vichekesho nchini, Anastazia Kisaveli, anayefahamika kwa jina la ‘Ebitoke’ kulalamika kwamba hapokelewi simu zake wala kujibiwa ujumbe mfupi pindi amtumiapo Ben Pol.

“Endapo nikimpenda msichana sifa kubwa huwa naangalia kujiamini kwake, pindi tukiwa tunaongea na kuchati, usafi wake, umakini na uharaka katika kujibu kitu au vitu ambavyo anaulizwa kwa wakati huo,” amesema Ben Pol

Mwanamuziki huyo kwa sasa anatamba na wimbo wake mpya alioupa jina la ‘Kidume’ ambao amemshirikisha msanii kutoka Nigeria anayejulikana kwa jina la Chidnma.

Na Brighiter Masaki

No comments:

Powered by Blogger.