Breaking News
recent

UN Yaitaka DRC Kutangaza Kalenda Ya Uchaguzi



Umoja wa mataifa umeitolea mwito mkali serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo kuhusiana na kutangaza haraka tarehe ya uchguzi na kuweka mikakati ya kuhakikisha uchguzi huo unafanyika katika mazingira yenye utulivu na amani.



Mkutano huo uliofanyika pembezoni mwa mkutano wa baraza kuu la umoja wa mataifa na ulioitishwa na naibu katibu mkuu wa umoja huo Amina Mohammed, pia mkutano huo uliobeba ujumbe wa umoja wa ulaya, Uingereza, Umoja wa Afrika, Jamhuri ya ushirikiano wa kiuchumi ya Kusini mwa Afrika, SADS, Jamhuri ya  nchi za Afrika ya kati na Kongo yenyewe.

Lengo kuu la mkutano huo lilikuwa ni kuja na mtazamo wa pamoja na kuhusisha wadau wote kuelekea uchaguzi wa amani na wa kidemokrasia nchini Kongo.

Na Kheri Yahaya Ramadhani

No comments:

Powered by Blogger.