Breaking News
recent

MANARA:OMOGI BADO NI KOCHA WA SIMBA

MANARA:OMOGI BADO NI KOCHA WA SIMBA
Timu ya simba  kupitia kwa msemaji wao Haji Manara imekanusha vikali uvumi uliokuwa ukienea kwenye mitandao ya kijamii juu ya klabu yao kuachana na kocha wake mkuu Joseph Omogi.
Akizungumza na kituo cha redio Efm katika kipindi cha E Sport msemaji wa timu hiyo amesema taarifa ya timu hiyo  kuachana na kocha wake mkuu sio za kweli bali  ni uvumi tu wa baadhi ya watu ambao hutumia mitandao ya kijamii kueneza taarifa za uongo, kuichafua klabu hiyo na kwamba klabu hiyo  hai ana mpango wakuachana na kocha wao huyo”alisema
  


Aidha msemaji wa timu hiyo ameiomba mamlalaka ya mawasiliano kuwachukulia hatua watu ambao wana tabia za kueneza taarifa za uongo kwenye mitandeao ya kijamii ili iwe fundisho kwani taarifa hizo husababisha taaruki na usumbufu  kwa watu 

 katika hatua   nyingine timu hiyo inatarajia kushuka dimbani  mwishoni mwa juma hili siku ya jumapili kucheza mchezo wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya stand  united ya mkoani shinyanga katika uwanja wa kambarage ikumbukwe kwamba katika mchezo huo timu ya simba inaitaji ushindi wa aina yeyote ili ijiweke nafasi nzuri katika msimamo wa ligi kuu hasa baada ya timu hiyo kutoka sare katika mchezo uliopita  
Na Hamadi hamadi

No comments:

Powered by Blogger.