Breaking News
recent

ASLAY NILIANZA PEKE YANGU NTAMALIZA PEKEANGU

MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva nchini Aslay Isihaka anayeongoza kwa kupachikwa majina mbalimbali na kufananishwa na wasanii wakubwa kimataifa, amesema kuwa baada ya kundi  la  Yamoto Band kuvunjika, yeye anaendelea vizuri na kazi zake wala hamna anachokikosa kwa sababu wakati anaanza hakuwa na kundi.


Aslay aliliambia Ebridensa kuwa alianza muziki akiwa peke yake na alikuwa na umri mdogo hivyo hata sasa ninauwezo wa kuendelea pasipo kuwa na kundi. Aslay ambaye kwa sasa anatamba na ngoma zisizohesabika kama vile, likizo, Baby Pusha, Nyakunyaku, Mhudumu na nyingine nyingi, alisema kuwa:

“Nilianza muziki nikiwa peke yangu na nilikuwa mdogo kiumri, enzi zile za ‘Naenda kusema kwa mama’, ila niliweza kufanya vizuri, kwa hiyo kuingia kwenye kundi na kutoka sioni kama nitashindwa kuendeleza muziki wangu. “Kwa sababu naona ni kama zamani tu, ndiyo maana nafanya vizuri, naachia Ngoma kila kukicha, na ngoma zangu kali na zinapendwa, mashabiki hawawezi kuzichoka kwa sababu mimi ni mwanamuziki mzuri, najua nini ninachokifanya, na sitegemei kushuka kimuziki”alisema Aslay

Aslay ni mmoja kati ya wanamuziki waliokuwa wakiunda kundi la Yamoto Band, kundi ambalo lilifanya vizuri sana ndani na nje ya nchini kupitia nyimbo zao kali kama Nitakupwelepweta,Cheza kwa madoido, Niseme Nisisema na Su waliyomshirikisha mwanadada Rubi.
Wasanii wengine waliyokuwa wakiunda kundi hilo ni Eneck Bela’The Base Maromboso na Beka Flavour.
Na BRIGHITER MASAKI

No comments:

Powered by Blogger.