Breaking News
recent

LULU AWAHASA VIJANA KUJIAJIRI.

Msanii wa filamu nchini Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameweka wazi kuwa huu sio wakati wa kutoa wito kwa vijana bali ni wakati wa kufanya kazi kwa bidii.

Akizungumza lulu alisema kuwa amechoshwa na kutoa wito kwa vijana wanaojibweteka majumbani kila siku kuwaambia wajishugulishe.
“Huu sio wakati wa kupeana au kutoa wito kwa vijana wasiojishugulisha na jambo lolote kama mtu anashindwa hata kutumia kipaji chake alichopewa na Mungu huyo tena basi , ni wakati wa kufanya kazi kwa bidii kwa watu wote ilikujipatia kipato kilicho halali.alisema Lulu


Aidha aliongeza kwa kusema kuwa nimejifunza kitu kuwa na biashara kubwa sio kuwa na pesa nyingi kidogo ulicho nacho ndicho kitakacho kusaidia wewe kufanya mambo makubwa mfano Ally Rehmtulah alisema kuwa yeye alianza biashara yake ya mitindo kwa kiasi cha pesa sh elfu 40.

Na Brighiter Masaki.

No comments:

Powered by Blogger.