Breaking News
recent

MOTO WATEKETEZA MAKAZI YA WATU 11 TABATA SEGEREA


Moto mkubwa uliosababishwa na shoti ya umeme umeunguza nyumba moja mali ya Bw. Hamis Rajabu pamoja na kuteketeza thamani zote na kuziacha familia hizo kutokuwa na mahali pakwenda.


Familia hizo zilikumbwa na kadhia hiyo siku ya Jumatatu wiki hii maeneo ya Tabata Segerea, ambapo kikosi cha zimamoto kilifika eneo hilo kwa jitihada za kutaka kuuzima pasipo mafanikio.”Sijui ni seme nini ilikuwa ni majila ya saa tisa alfajiri ghafla nikasikia kelele za wapangaji nikatoka nje kutaka kushuhudia lakini ulikuwa moto mkubwa  ukitoka katika soketi bleak” Alisema Hamis.

“Siwezi zungumzia kwa sasa nikiasi gani cha gharama zilizowezakuteketea katika ajali hii kwani nimapema mno kuelezea tukio hilo”. Alisema Hamis

Baadhi ya mashuhuda wa ajari hiyo Hamza Ramadhani alisema “moto ulianza kwenye soketi bleka na kuanza kusambaa nyumba nzima tulijitahidi kadri ya uwezo wetu kuweza kuokoa baadhi ya mali lakini moto ulituzidi nguvu,Hata hivyo dereva wa gari la zimamoto alielezea baadhi ya changamoto zilizopelekea kushindwa kufanikisha kuuzima moto huo ni pamoja na miundo mbinu ya maeneo hayo kuwa mabovu kwani nyumba hazipo katika mpangilio wa kuruhusu magari makubwa kuweza kupita kwa urahisi zaidi. 

By Hance Mwaisemba

No comments:

Powered by Blogger.